TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA POLISI TANZANIA - 2025
Jeshi la Polisi Tanzania limetangaza nafasi za ajira kwa vijana wa Kitanzania wenye sifa zinazotakiwa.
Sifa za Muombaji
- Awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa, pamoja na wazazi wake.
- Awe amehitimu Kidato cha Nne au Sita kati ya mwaka 2019 hadi 2024.
- Wenye elimu ya Astashahada, Stashahada au Shahada wawe na umri wa miaka 18-30.
- Kidato cha Nne wawe na ufaulu wa Division I-IV (kwa Division IV, wawe na alama 26-28).
- Kidato cha Sita wawe na ufaulu wa Division I-III.
- Awe na urefu wa angalau 5’8” (wanaume) na 5’4” (wanawake).
- Awe na kitambulisho cha Taifa (NIDA) au namba ya utambulisho.
- Awe na afya njema kimwili na kiakili, hajaoa/kuolewa, na hana alama za kuchora mwilini (tattoo).
- Awe tayari kuhudhuria mafunzo ya Polisi na kufanya kazi mahali popote Tanzania.
- Asiwe na historia ya uhalifu wala matumizi ya dawa za kulevya.
Utaratibu wa Kutuma Maombi
- Barua ya maombi iandikwe kwa mkono na iambatishwe kwenye mfumo wa PDF.
- Maombi yafanywe kupitia tovuti rasmi ya Jeshi la Polisi: https://ajira.tpf.go.tz
- Maombi yote yawasilishwe kabla ya tarehe 4 Aprili 2025.
Fani Zinazohitajika
- Uhandisi (Civil, Electrical, Mechanical, Marine, Computer, etc.)
- Sayansi ya Afya (Medical Doctor, Nursing, Pharmacy, Physiotherapy, etc.)
- Teknolojia ya Habari (Cyber Security, Software Engineering, ICT, etc.)
- Lugha na Mawasiliano (Journalism, Translation, Sign Language, etc.)
- Masuala ya Sheria na Usimamizi (Law, Tax Management, Real Estate, etc.)
Kwa orodha kamili ya fani zinazotakiwa, angalia tangazo rasmi.
Maombi yote yasiyofuata utaratibu hayatazingatiwa!
Kwa maelezo zaidi, tembelea tovuti ya Jeshi la Polisi Tanzania.
TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA ZA JESHI LA POLISI TANZANIA - 2025
Bofya hapa kuanza Application